MOURINHO ASEMA TERRY ATABAKIA NAHODHA WA CHELSEA KWA JUHUDI ZAKE.


MENEJA mpya wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedai kuwa John Terry atabakia kuwa nahodha wa timu hiyo na kukataa kuweka wazi kama anataka kumsajili mshambuliaji nyota wa Manchester United, Wayne Rooney. Terry mwenye umri wa miaka 32 alikuwa nahodha wa kikosi cha Chelsea kilichonyakuwa mataji mawili ya Ligi Kuu nchini Uingereza wakati Mourinho alipokuwa kocha mara ya kwanza. Lakini pamoja na kuwa nahodha kwa muda wote huo Terry hakuwa chaguo la meneja wa mpito Rafael Banitez kwasababu ya majeraha ya mara kwa mara yaliyokuwa yakimsumbua katika msimu wa 2012-2013. Mourinho amesema hana tatizo na terry kuendelea kuwa nahodha wa klabu hiyo lakini itabidi afanye kazi ya ziada kuhakikisha anakuwa na namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza. KOcha huyo mwenye maneno mengi aliendelea kusema kuwa wachezaji ambao walikuwepo katika kipindi chake cha nyuma alichokuwepo hapo wasitegemee mteremko kutoka kwake kwani viwango vyao ndio vitawafanya wabakie katika kikosi chake.
Share this post :
https://www.facebook.com/hassani.haji

Follow me on instagram

https://www.instagram.com/hancyclassics/

Follow Me Insta

A photo posted by hancyb (@hassanaly_b) on

 
Support : hassani bakari haji | +255755537543 | +255712919980
Copyright © 2016. hancyclassics - All Rights Reserved
Template Created by hassani bakari Published by hassani bakari
Proudly powered by hassani